Ubelgiji kuelekea kombe la dunia


Wakati wa michezo ya kuwania kufuzu fainali za kombe la dunia za mwaka huu, Ubelgiji iliweka rekodi ya kufunga mabao 43 na mshambuliaji wao hatari anaeitumikia klabu ya Man Utd Romelu Lukaku aliweka rekodi ya kuwa mfungaji wa muda wote katika nchi hiyo.
Mpaka sasa Lukaku amefikisha mabao 33 akiifungia Ubelgiji, hali ambayo inatazamiwa huenda ikamuongezea morari ya kufanya vyema wakati wa fainali za kombe la dunia zitakazoanza rasmi Juni 14 nchini Urusi.
Kocha mkuu wa timu ya taifa la Ubelgiji lenye watu zaidi ya 11,358,357 Roberto Martínez, ana matumaini makubwa na kikosi chake, kutokana na uwepo wa wachezaji wenye uzoefu wa kupambana.

Maoni