REAL MADRID KOCHA WAO HUYU HAPA WAMTANGAZA RASMI

Klabu ya Real Madrid imeshangaza umma baada ya kumtangaza kocha wa Hispania Julen Lopertegui kama kocha wao mkuu mpya mtarajiwa atakayerithi mikopa ya Zidane aliyoiacha baada ya kutangaza kujiuzulu mapema baada ya kutwaa ligi ya mabigwa Ulaya.

Pichani: Lopertegui akiwa na timu ya hispania.

Hata hivyo Real Madrid wametimiza ahadi waliyoitangaza baada ya kusema watamtangaza kocha mpya kabda ya kombe la Dunia.Julen yuko na kikosi cha Hispania kwa sasa Urusi akikiweka vizuri kwa ajili ya kukipiga dhidi ya Ureno jumamosi hii.

(TANGAZO) "TUNATANGAZA MATANGAZO YOTE PICHA ,YA VIDEO ISIYOZIDI DAKIKA MOJA NA NUSU,NA MANENO PIA KWA BEI RAHISI SANA HASA KIPINDI HIKI CHA KOMBE LA DUNIA SIKU MARA TATU NA BONUSI YA KUTANGAZWA KWA SOCIAL MEDIA ZETU ZOTE WASILIANA NASI KUPITIA 0716243875"

Kocha huyu ataitumikia klabu hii kwa mkataba wa miaka mitatu atakaosaini baada ya kombe la Dunia,Mabigwa hawa mara tatu mfululizo wa ligi ya mabigwa Ulaya wana hamu ya kumpata mrithi kama Zidane.

HABARI na  Prosper Barthalomew.

Simu:255716243875.

baruapepe:barthaprosper@gmail.com

Maoni