MORROCO IMEKOSA KITU KIMOJA TU

Morroco ametolewa kiume lakini watu wanaweza kupinga maneno yangu haya lakini naenda kuwaonesha tofauti kati ya Morroco soka lake na mataifa mengine shiriki kutoka Afrika.

Mpira ni magoli Ronaldo alishidwa kushikwa vizuri dakika ya nne kwa mpira wa kona na kupiga kichwa na kufunga.Basi Morroco alifanya kila kitu na kushidwa ni wana nidhamu ya mpira kuucheza wamecheza kati ya soka nililolifurahia katika mashindano haya ni la Morroco wana bidi wajiongeze katika utiaji mipira wavuni.

Morroco walipoteza dhidi ya Iran lakini uzembe wa kutia mipira wavuni ndo lilikuwa kosa kubwa mpira ameucheza akipoteza kiungo ya Ureno na kusukuma mashambulizi hatari licha ya kutofunga magoli.Morroco pengine ametolewa kutoka na mechi ya kwanza ya muhimu kupoteza ambapo ile mechi ilikuwa( must win game) kwa goli la kujifunga.

Winga wanacheza mpaka raha utumiaji wa nguvu na ushambuliaji wa Amrabat unafurahisha na kutia presha katika ngao ya ulinzi katika timu pinzani anakaba na kushambulia na ana spidi ana toa pasi na kubishana na mabeki kwa nguvu zake.

Nafikiri Morroco akiendelea  na soka hili ana huduma ya beki safi Hakimi Archuf na Aminie Harit ambao wote ni vijana wana nguvu za kutumika katika mashindano yajayo ya Afcon na wakashinda na huu uwezo wao wa vijana kucheza soka ulaya wanabidi wafurahie na kuwatumia katika mashindano mengine.

Kombe la  dunia/ uchambuzi na Prosper Bartholomew

Simu:+255716243875.

Barua pepe: barthaprosper@gmail.com


Maoni