NAE CRYSTAL PALACE KAIGA MFANO WA SPURS ,CHELSEA,ARSENAL, NA WEST HAM

klabu ya Crystal Palace wameridhia kuongeza kiwanja cha selhurst kufikia mipango mipya.

Mipango yao mipya  wameweka hadharani ikiwa kiwanja kitaongezeka Uwezo wa mashabiki utaongezeka mpaka watu 34,000 na utakamilika baada ya miaka miwili ndani ya uwanja huo kutakuwa na majengo ya shughuli mbalimbali za kijamii

Mipango yote ya kuhusu ukuaji wa kiwanja cha selhurst kitawasilishwa kwa baraza la Croydon tarehe 18 januari 

Vilabu mbalimbali vya London vimekuwa vikipanua na kukuza viwanja vyao kiwanja cha Spurs kinajegwa hivi sasa, Chelsea wanaanza msimu ujao kujenga kukipanua Stamford bridge ,Arsenal wanatumia Emirates na ni kiwanja kikubwa  na West ham nao wako London uwanjani, kiwanja kikubwa nacho. 

Maoni