ISHU YA DAVID LUIZ YANUKIA REAL MADRID

Klabu ya Real Madrid inafanya lolote kuisaka saini ya beki wa kati Mbrazili David Luiz ambaye ana mahusiano mabaya na kocha wa Chelsea Antonio Conte

Ugomvi huu ulianza pale kwenye suluhu ya 3-3 dhidi ya Roma ambapo luiz akufurahishwa kutolewa . doa liongezeka alipoachwa nje kwenye mchezo dhidi ya Manchester united hali haikuwa shwari sana alipocheza dhidi ya FK Quarabag na ilizidisha hofu kuachwa benchi kwenye mchezo dhidi ya West brownich Albinion na Liverpool

kocha wa Chelsea mwenye umri wa miaka 48 akiwa amefundisha timu za Juventus na Italia kwa mafanikio amesema luiz atakosa mchezo dhidi ya Swansea kisa majeraha pia alionekana akifanya mazoezi mwenyewe wakati ugomvi ulipokolea
Beki huyo mwenye miaka 30 alirejea klabuni hapo akitokea PSG na kuwepo kwenye PFA kikosi cha msimu . alikuwa nguzo muhimu ya kuipa Chelsea ubigwa msimu uliopita.

Maoni